Kutengeneza pesa kwa kutumia Facebook
Imekuwa ni kawaida kwa watumiaji wengi wa mitandao ya
kijamii kuitumia kuelezea mambo mengi sana. Wapo wanaozungumzia masuala ya
kijamii, kiafya, kisiasa, kiuchumi, mahusiano, elimu za dini na kidunia, muziki
na mambo mengi mbalimbali. Lakini leo nataka tuangalie jinsi unavyoweza kutumia
mtandao wa facebook kutengeneza hela.
Kuna msemo wa Kiswahili unaosema kwamba “Biashara ni matangazo” msemo huu unakuwa
dhahiri pale tunapoangalia barabarani mabango mbalimbali, matangazo kwenye
television na hata kwenye mitandao ya kijamii. Watu wanatumia akili nyingi kutengeneza
picha za kuvutia macho ya watazamaji au kutengeneza hata vikaragosi “Cartoon”
vinavyotolea maelezo bidhaa zao. Je, vikisha tengenezwa hupelekwa wapi?
Baada ya kutengeneza picha zako za matangazo au vikaragosi,
unaweza sasa ukasambaza kwenye mitandao ya kijamii na kuwafikia wateja moja kwa
moja. Kwa kutumia facebook unaweka picha yako kwenye account yako au unaweza
kutengeneza ukurasa ambao wenyewe utakuwa mahususi kwa kutangaza tu biashara
unayoifanya. Lakini pia kuna makundi mengine mengi kwenye facebook ambayo
yanafanya biashara kama ya kwako, hivyo unaweza kuingia kwenye kundi ambalo
linazungumza masuala ya biashara na wewe ukaweka biashara yako.
Jinsi ya kutengeneza ukurasa wako wa facebook. Bofya hapa……kisha
fuata maelekezo.
Baada ya kutengeza ukurasa wako wa facebook unaweza ukaupa
uwezo wa kufikiwa na watu wengi kwa kasi na urahisi Zaidi kwa kufanya baadhi ya
mambo ili kuupa uwezo.
Kitu cha kwanza ni kuupa uwezo “boosting page”, hii
hufanyika kulingana na mahitaji yako binafsi. Unalipia kiasi cha pesa, kuanzia shilling
6,600/= za kitanzania na kuendelea. Hii inatokana na idadi ya watu ambao
unahitaji kuwafikia.
Pia unaweza kutengeneza tangazo yaani “Facebook Ads” ambapo
facebook wenyewe watakuwa wanakutangaza kulingana na watu amabao unachangia nao
vitu unavyoviweka kwenye mtandao.
Kutengeneza pesa kwa kutumia Facebook
Reviewed by Unknown
on
05:20:00
Rating:
Reviewed by Unknown
on
05:20:00
Rating:
